NA DENNIS MURITHI
Wanafunzi wa vyuo vikuu humu nchini husema kuwa wanafurahia maisha ya shule kwani huwa hawanyimwi ruhusa ya kutenda jambo lolote wanalofikiria linawapendeza. Hapo ndipo utapata ya kwamba wengi wao wanajiingiza katika maisha ya anasa na kusahau kilichowaleta chuoni. Hata kama ni vigumu kwa walimu wao kuwarekebisha, ni vyema wawafanyie mafunzo na maelekezi ya jinsi wanavyofaa kuwa na maadili na kuachana na tabia duni ambazo hatimaye zinawadhuru katika siku za halafu.
tusije tukawalaumu chipukizi hawa pekee,wazazi wao pia walifeli katika kuwaelekeza wanachostahili kufanya katika mazingira mbalimbali.ndipo wahenga waliponena bila kukosea asiyefunzwa na ulimwengu hunzwa na ulimwengu.
Advertisements